LYRICS

Search for a song or choose an album and track.

A FATHER FIGURE album cover

A FATHER FIGURE

Dizasta Vina

A confession of a mad father

A FATHER FIGURE • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Nilimwambia hakuna kitu ataniambia Nikifa hakuna kitu nitamwachia Nilimwambia anaitia aibu familia Nilipenda mtoto ila tangu nimzae nilijutiaNilimwambia anastahili fimbo Anastahili msiba mbaya usio na maziko Asikae mezani asishike sahani au kijiko Asitumie jina langu la mwisho Nilimchukia sanaNilimwambia asiniite baba Aliponiita hata bahati mbaya nilimchapa Sikumpa mahitaji, hamu ya mtoto iliniisha ghafla Alianza shule sikulipa adaWaliponiuliza nilimkana hadharani Nikasema hata kufanana hatufanani Nilimwambia simpendi ni bora ningezaa hata Nyani Nilitamani nimgawe kwa jiraniNilimpeleka kwenye misa za kilokole Nilimchapa viboko vya kutisha kwa Mkole Habari zake zilitambaa nilipewa pole Nilihama mitaa kuepusha watu kuninyooshea vidoleNilimuwekea mifano kadhaa ya kubuni Kwamba kuliko yeye bora ningezaa hata Mhuni Nilimwambia namwona kama Chawa au Kunguni Aliniponigusa bahati mbaya nilinawa kwa sabuniSikumpenda nilihamishia chuki kwa Mama yake Niliona laana kuleta mtoto wa aina yake Sikutaka kumwona wala kumjua katu Na nakiri Nilishajaribu kumuua mara tatuHakuwa na marafiki tulimtenga ndugu Tuliamini ilikuwa ni laana toka kwa Mungu Alinikimbia sikutaka kusikia sauti yake Sikuwa tayari kuuafiki utofauti wakeTulimweka kwenye taasisi bila idhini Alelewe akifanyiwa uhakiki wa kidini Kilichofanya nimwone ni mzigo mara mbili Ni pale taasisi zilipomshindwa kumbadiliTofauti ya haiba na hisia Sikuwa tayari kamwe kuukubali uhalisia Achana na vipigo vikali kumnyima chai Ilibakia kidogo nimzike akiwa haiNilikomaza chuki kwa kutumia jadi na dini yangu Au itikadi ya jamii yangu Nilifurahi kuona hana mahala pa kwenda Maana sio marafiki hata ukoo ulimtengaHawakutaka wakae naye Vitabu vya Mungu vilishauri auwawe Nilikesha kuomba Mungu aibadili tabia yake Alipopita karibu nilimtemea mateNilimwita majina ya kutosha ya kishezi Mara boga mara mboga mara shoga mara ndezi Mara mzoga, Nyoka asiye nyooka kwa malezi Nilitamani hata nafsi ingemtoka niimbe tenziNiliamua kufanya maamuzi magumu Nikamfunge porini kisha nimnyweshe sumu Nikaandaa nyezo nikanunua na kamba Nikaenda chumbani nikakuta barua kwenye kitandaInasema Mi ni mtumwa wa maumbile kiasili Iliyonizidi nguvu kihisia kiakili Natamani ingekuwa rahisi kubadili Na kwa bahati mbaya Baba hukuwa tayari kujadiliNisamehe sana baba Muda hautoshi kukuomba msamaha mara saba Kwakuwa nimeshindwa kuwa jinsi we unataka Najitoa uhai ili nikuondolee dhihaka

More From This Album

More songs from this album

Join The Family

New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.

© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.