LYRICS

Search for a song or choose an album and track.

A FATHER FIGURE album cover

A FATHER FIGURE

Dizasta Vina

A father figure (Official album intro)

A FATHER FIGURE • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Natazamwa kama mgongo Wa kuegewa kama chombo Nikitegemewa na watoto Lakini kwa ndani mi' ni mtoto piaMtoto wa katikati Njiapanda kati ya Ukweli na uongo Ukubwa na udogo ama Upofu na uchongo Ama pumbazo na mwongozoKatikati ya uhalisia Na mategemeo Karibu na jitihada Mbali na egemeo Sina hesabu ya mafanikio Kila kitu ni jukumu na uwepo wangu Ndio hukumu yangu ya leoSina cha thamani nilichorithi Ila nilichonacho ni kumbukumbu ya simulizi Na picha nilizokuwa nazo Nilizopewa na wavuja jasho Wasakatonge wa mwanzo kwahiyo Nigawie masikio yakoMacho yalinipa tishio lenye manufaa kwangu Maana nilishuhudia kufanikiwa na Kushindwa kwa mashujaa wangu Lakini shuhuda zilinifunzaZilinifunza kuhusu Mashujaa Wa karibu na mbali Wenye nasibu za ghali Au watabibu wa kuponya hali Na nguvu ya kufukuza shali Za wadhalimu na waharibifu Wenye visu vikaliMashujaa walisisimua sana Lakini wapo kadhaa waliokufa Na hawakuacha alama Nilifunzwa kuhusu hawaHawa mashujaa walipanda maua Wakilea vyema yakachipua Na wengine usingizi ulipowachukua Wadudu wala mizizi wakafukuaMachache yaliyofanikiwa kukua Ndege waliyachukua Na mengine hayakuwa mahala pema Kwahiyo yalichomwa na jua na kuunguaOooh hujui walimwengu walisema nini Kuhusu hawa mashujaa wangu walioshindwa Walisema Kaharibu Kwakuwa shujaa kwa walimwengu Ni yule anayeweza wakati wa kufanya Lakini sio anayeshindwa wakati akijaribuKwa walimwеngu shujaa Ni yule mwenye nguvu Asiyеtoa chozi wakati wa uchungu Asiyekosa au anayeonekana mtukufu Kwa walimwengu ushujaa ni Kuweza na sio kuthubutuKwahiyo wakati sherehe za mashujaa Wao zikipikwa kuchochea Hadithi za mashujaa wangu Zilizikwa na kupoteaKwakuwa mashujaa wangu Hawakuvaa suti zenye nakshi na kuita Hawakuwa na viatu vya kung'ara hivyo Hawakupendeza kwenye jaridaNi kama walipima ushupavu wa mashujaa Kwa kuangalia afya za maua Bila kujua afya za maua sio ubora Wa anayeyajua pekee Lakini kuna jua na mvua na ni Ubashiri wa kujua lini vinakuja Uhakika wa kesho, kesho yenye giza Na hakuna anayeitambuaShujaa wangu alileta mlo mmoja Kuhakikisha siku haipiti, na aliweka Tofali moja wakati wa kujenga msingi Alifagia barabara alipambana na Uraibu kama kamali, ulevi na madawa Ila hadithi yake haikuvutia gazeti Sio sawaNi vile nimeanza kuwa kama shujaa Wangu nimegundua kuwa sijamaliza kujua Ni kama nimeanza kulea wakati sikumaliza kukuaNatamani kuwa shujaa mzuri Lakini nipo hapa kujifunza Na pa kuanzia sipajuiSipajui maana maelekezo ni mengi saa hii Mara jikaze wewe, baba halii Mara utapoteza nafasi, watu hawatanii Mara kwanini usifanye kama nanihii Ona mtoto wake amenanihiiBahari ya elimu ni pana kuushinda upeo Kulia matarajio, kushoto mategemeo Bado najifunza sipo mbali Ila sijui lini nitakuwa tayariInaniwia kuweka kipimo Cha kujua kipimo kiundani Kupima usahihi na wito Ninaposema hadharani Unawaandaaje watoto kwenda mitaani Kwa sababu kuliko kuwa mkata maua vitani Ni bora kuwa mwanajeshi kwenye bustaniNini maana ya kuwa baba Ikiwa bado najifunza Kutosherehekewa nikishinda Ila kusakamwa nikianguka? Hata nikipendwa au nikichukiwa Ni sawa ila si vyema nikapuuzwa Nimechelewa ila ni vyema Nimejua kuwa baba hazaliwi Anaundwa

More From This Album

More songs from this album

Join The Family

New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.

© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.