LYRICS

Search for a song or choose an album and track.

A FATHER FIGURE album cover

A FATHER FIGURE

Dizasta Vina

Hatia VI

A FATHER FIGURE • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Salamu baba mi mwanao Naandika waraka kwa maana hutaki vikao Nahitaji majibu nikihisi ni haki yangu Najisikia vibaya kusikia unaishi na sina ngaoNimeshika kalamu haya maandiko Yametoka mahala timamu palipo wito Sijatumwa na wenzangu hii ni akili yangu mwenyewe Waraka huu ni salamu zangu za mwishoNina akili najua mambo yanapokuwa mrama Natambua uhalisia nazitambua njama Pengine nitachokisema kitazua laana Nitaibeba lawama kwa kujifanya najua sanaNdugu zangu wanachosema sisawiri Mpaka wanahisi nimeanza kuchezwa na akili Hata wakitaka kunitenga sibadili Ulinitenga jana siogopi kutengwa mara mbili babaMajirani wanatamba kukuongelea Wakisema sina baba na kazi ya kukusemea Na ukweli ni kwamba ni utata sana kukutetea Maana shida ilinibana na baba haukutokea jeUtachukia nikiegemea penye power Au utanipa hatia mikono michafu niende nawa Nipo mbele yako kamwe siigizi uwepo kama wewe Basi jibu kero zangu twendе sawaJuzi nilikuhonga maua, Jana nikakuhonga na tena Subira gani isiyo na heri shaabash Nimechoka kuchomwa na jua Jionyеshe leo nimechoka barua Nimechoka baruaBarua zako zinahubiri ushindi Kutangaza vita wakati mtutu tu haushiki Na cha ajabu maadui ni wa kurithi Chanzo ni kitendawili nilichokisoma kwenye hadithiNjoo ulee wagonjwa ndo' uongee kuhusu upendo Tuvae bendera moja ndio uongee kuhusu uzalendo Msamehe aliyekufanya uondoke ndo' uendeelee Kuhubiri kutubu kuhifadhi na kusameheJenga daraja baba mahusiano yanavunjika Hamna faraja huoni wanao wamekaza ndita Jenga imani tena kwa wote waliogadhibika Jenga kama ambavyo uliijenga hii nyumba kwa siku sitaHaukuja tulipopita kwenye Miaka 400 ya utumwa njaa maradhi vita giza nene Nipe sababu moja vipi nikujali vipi nikupende Sababu moja tu kukusikiliza weweNyumba uliyotupa ina twiga ina ndovu Majirani warembo wenye figa na vitovu Vinavutia, kuna dhahabu kadhalika Zinatutajirisha ila zinafanya tuwe waovuHuu uchafu atatetea wakili gani Siri ipi na asili zetu hazilingani Japo akili mali sio siri asili ghali Tunamwagana damu kugombea rasilimaliTunaisha kwa wivu wetu Tunasita kwa uvivu wetu Tunazikwa na mbinu zetu Tunapikwa na kinu chetuTunasita kushika insha Tunapitwa na wapita njia Umoja unavunjika huku Tumeshikwa na simu zetuSina tofauti nna watoto kama wewe Napata changamoto kama wewe Kama soja kwa ajili yao napambana naposhindwa Tunateseka pamoja Kwani sina roho ndogo kama weweAsante kwa ulezi dhanifu Asante kwa kuniandikia sheria za kishenzi Kwenye pegi nadhifu asante kwa kuniacha stendi Nikisubiri mapenzi ya ahadi nakesha nikienzi wasifuAsante kwakuwa mbali nami Kiasi nina shaka kuwa haujui nina hali gani Umeacha barua ndefu ambayo sijui kama yako Au ya kufoji na bado inahitaji mkalimaniOna Napanga mipango ya kijinga Ona naghafirika nafanya uliyopinga Ona napinda napika chuki wenzangu Wenye nyumba ndinga maana mimi ngano tu inanishindaHuko mbali umejitenga nashanga Haujui kinachosemwa na jamaa Haujui usafi ni ndoto, ndoto iliyotengwa na ridhaa Haujui ni ngumu sana kuwa mwema ukiwa na njaaHaujui kuhusu adha za dunia Haujui kero maana maudhi yalipokupata ukakimbia Haujui kuhusu kifo na magonjwa haujui kuhusu Insha na maandiko haziwezi tibu hivi vidondaNdugu zangu umewajenga kwa vpaji Wapo kadhaa umewapa pesa za mitaji Wengine warembo wenye vyeo wenye hadhi Sisi tusio na hali tulalamike kunyimwa hakiImechafuka taswira inaenda slow focus Pengine its all bogus Pengine I'm mad And I'm talking to my own consciousLabda haupo ni hadithi tu Na kama ulifikia kifo ufalme umefika mwisho Haurudi tena so nawaza Lini utakuwa mwisho wa uhanithi huuUzazi sio simple but I still care Nina watoto shida zipo and I'm still here Matatizo yanapokaba kwenye shingo sikimbii Napambana mpaka mwisho like a real manSio kosa langu kutokuwa na uhakika upo SikujuI sura maana hauna picha Google Nipe ishara kuwa unaishi hata nikituma Bakshishi niwe ninajua kuwa zinafika hukoWenye majoho rangi nyeupe na dhahabu Wana barua zako za tafsiri za kiarabu Wanasema wanakujua kuliko ninavyokujua Nikiwatilia shaka wananiita mwanaharamuJe ni kweli uliwapa uwakilishi Ni ngumu kuwasadiki hasa ukiwadadisi Kama wanaongea uhalisi au wanachonga sera Sometimes hawafundishi wananiomba helaThibitisha hizi hifadhi si uwongo Uliowaacha wana nishani za uozo Wakificha sura kama ulivyoficha wewe Utawaadhibu kwa maji na moto Wakati unahubiri msamahaNina maswali bado Halahala sikukemei Nashangaa wenzangu wanakesha Wakiimba utukufu wa dhambi zako Au ndo' mkubwa hakoseiNimeelemewa na dhambi Baba mzazi unasema sina hadhi Unajua wasifu unajua majibu Umenizaa dhaifu unategemeaje niwe msafiKwanini usije ili tujue moja Uuonyeshe uso wako ili tufunge hoja Kwanini usijionyeshe tufurahi nafsini Tujue kipi halisi kipi sogaWanao wanaweka mipaka wakivutana Wanabishana kila kikao wakikutana Wameishi bila uwepo wako juzi na jana Swali ni kwamba utaonyesha hasira wakikukanaUlinizaa kwa matakwa yako Nilisimama kwa ajili yako ni zamu yako leo usimame kwangu Sina usafi kama wako hautaki nilitaje jina lako Kwanzia sasa usilitaje languNilihitaji jibu moja tu sio picha mia Umeamua kujificha so najificha pia Nimekutafuta vya kutosha nimechoka Nipo hapa ukinihitaji unajua pa kunipata dear..father

More From This Album

More songs from this album

Join The Family

New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.

© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.