–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

A FATHER FIGURE
Dizasta Vina
The last confession
A FATHER FIGURE • Dizasta Vina
Lyrics copied!
"Baba, let me get this clearly, ni wewe kweli umefanya hivi? Na kama ni wewe, ni kwanini ulifanya hivi? Unajua, hatuwezi kukusaidia. Sio dada Mori au kaka Levo, ikiwa hatutajua the real story"Nilipozaliwa nilijua ulimwengu ndio utanionyesha dira
Sikujua dini wala kabila
Sikuwa na itikadi desturi wala mila
Wala chama, niliujua upendo kabla ya hiraNilionyesha tabasamu hata kwa ambaye simjui
Kabla ya ulimwengu haujanipa maadui
Kabla sijajifunza kuchagua
Niliujua umoja na ulimwengu ndo' ulionifunza kubaguaNafsi haikuweza kutamani
Nilifundishwa pesa ina thamani
Kabla ya utu, nilijali nilimpenda Mkyuba na Mjerumani
Hata kubagua rangi nilifunzwa tu ukubwaniSikutunza kisasi nilipofanyiwa njama
Ya dunia yalinighasi nikamkimbilia mama
Jamii ilizembea walimwengu wakashindwa kunikanya
Na wazazi wakanitishia laanaSikuujua uongo sikuujua ufitini
Nilifunzwa na hii dunia sikuwa mchoyo kwa idhini
Dunia ilinipa ndugu wakanidhamini
Kabla kunifundisha utu wakanirithisha diniNiliigawa thamani kwa kuzingatia upendo
Kabla dunia haijanifunza kuutamani urembo
Wakati mdogo sikuijua mipaka ya wahisani
Nilivunja nikaenda kucheza mpaka kwa jiraniEeh!! Sikuona ishu aisee
Kumbe jirani alikuwa na bifu na mzee
Mzazi alinipa kula sikuweza kuihoji haki
Bila hatia nikashiriki ugomvi wa wazaziNdipo nilipoijua chuki
Nikajua maana ya mipaka ya Marekani na Urusi
Sikujua kuongea nikapewa lugha ya Matusi
Na kabila la Kihutu ili nimtukane MtutsiNikamjua ndugu wa upendo anaitwa wivu
Nikayajua majivuno kisha hasira kisha bifu
Nikafichwa ustaarabu nikafichwa haya
Nikapewa nguvu za miguu niende kuutimiza ubaya"Ah Baba, unajua unaweza kwenda jela miaka mingi sana?
Hivyo kuwa direct basi. Ukiweka pembeni falsafa zako, tunahitaji utuambie ukweli
Why? why uliamua kufanya hivyo? ehh? kwanini yaani?"Asili imenipa macho nashukuru
Nione mabaya matamu nione mazuri yanayonidhuru
Wazuri wanaojiremba niwapende
Ili nitoe jasho kisha nije niwape pesa wanitendeUjirani uko wapi? siku hizi hatuchezi pamoja
Hatupigi soga tunawekeana mageti
Ah hakuna kuombana chumvi
Kwakuwa kuna fensi ukuta mkubwa na vihunziTunafuga vikosi vingi vya kininja
Mbwa na majeshi na walinzi kujilinda
Mwanzo niliogopa simba
Sasa nafunga mlango maana hata binadamu ananiwindaNimekubuhu nimekinai maudhi
Naona mstari mwembaba kati ya uhai na mauti
Sikuchagua hasira au kinyongo kunishika
Nikalambisha udongo watu sitaWa kwanza nilimpiga risasi mara tatu
Sikuuliza maana hakuvaa gwanda kama langu
Kiongozi akasema nisipigwe na bumbuwazi
Kutoa uhai wakati wa vita si uuajiNikajuana na mtu wa pili
Mungu wa dini yangu alimwita huyu kafili
Tulichukiana kiasi alitaka kunipiga
Nikamuwahi maana imeandikwa vita ni vitaWa tatu alisahau chake changu changu changu
Njaa yake ilimleta kwenye shamba langu
Nikamkamata nikamziba mdomo asilete methari
Nikamfungua macho na sikio aujue ubepariWa nne na watano waliniletea ushenzi
Cheo kilikuwa kidogo wakati tulikuwa wengi
Ili wasije kufukua maiti, nikamuua wa sita
Alikuwa shahidi
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.