–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

A FATHER FIGURE
Dizasta Vina
Theluji
A FATHER FIGURE • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Anachota kwa vidole viwili
Anachemsha kwa kijiko inanawili
Inakuwa nyevu, anachukua bomba la sindano anaivuta
Inajaa kisha anadunga mwiliAkili inahama anaita stimu
Ladha tofauti, sawa na sukari na ndimu
Kila stimu ikiisha anajiongezea
Anazoea mwili unanasa anaanza kubobeaAnajaribu kuacha anairudia
Mwili unamlilia uraibu unamvizia
Hataki uhalisia maana haujamvutia
Anajianzishia uhalisi bandia
AnasemaMwili unapoa akili inatosha tufani
Kihali gani chombo akidondoka rubani
Alitaka furaha, furaha imegota tutani
Dawa inampa amani, amani aliyokosa nyumbaniAnapoteza sura ya kisomo
Anapoteza kazi, hamu ya chakula na ngono
Raha anayoipata inakuwa siri yake
Kiasi anauza mali kukidhi haja za mwili wakeMuuzaji anaendelea kuuza
Serikali inaendelea kuzuga
Jamii inaendelea kuvunga
Washikaji wanaendelea kuvuta
Mtaa unaendelea kufaUsimuuzie madawa mwananguNajua hii kazi inakupa mafao
Tafakari yatamkuta mwanao
Usimuuzie madawa mwananguStarehe yake mpya inamvunja pochi
Inamaliza afya lakini inamfuta chozi
Inamweka mahala pasipoguswa na Mwokozi
Bahati mbaya damu inawasha anakuna ngoziTheluji inamfikisha mbinguni vyema
Anaihusudu hali
Kiasi anashuka anaiba mpaka mali ili arudi tena
Anaisujudu ganziAlikuwa na mchumba
Wali-share all the nice things you know?
Dinner dates Ice creams
Walienda kwenye bata za mjini, kumbi za movie
Kuangalia sijui The black Panthers sijui The VikingsLeo yupo ila hatamaniki
Haangaliki
Bora angekuwa malaya au mlevi wa bapa nyingi
Ningeelewa, leo ngada zinamfanya anakata ringiWanasiasa wanabishana
Mchungaji ibadani na Polisi ofisini
Wafanyabiashara wana idhini
Na mtaani madawa
Yanaendelea kuwalaza chini vijanaNajua biashara inakupa mafao
Kiasi kwamba unawaza jinsi ya kutupa mbachao
Lakini usimuuzie ngada mwanangu
Labda kesho yatamkuta mwanao, just think about itLabda hauna elimu sana
Naomba tuongee ka' wazazi maana
Nimeuchoka huu ubazazi
Unaofanya nahisi umepitwa na wakati
Na unajua nakuheshimu mwanaSina nguvu ningekupeleka mahakamani
Ila uchumi wetu haufanani
Mpambanaji leo nashindwa vitani
Namzika mwanangu 'asa mi' nitazikwa na nani?Swali, una nguvu? Ndio
Haufanyi chochote kutafuta suluhu? Sio
Hauko mahabusu, familia yako tukufu
Kwa hiyo unahisi haya mambo hayakuhusu, au sio?Usimuuzie madawa mwananguLabda hii kazi inakupa mafao
Tafakari yatamkuta mwanao
Just think about it
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.