–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

A FATHER FIGURE
Dizasta Vina
Wachezaji wa timu
A FATHER FIGURE • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Wanasema duniani kuzimu
Kwanini ukeshe kushika protocol wakati
Ulaji muhimu
Watu wanachohifadhi ni mbinu
Kucheza kulia kushoto ila wote ila wote
Ni wachezaji wa timuChumba kilijaa njemba za kisasi
Walipanga vifaa ka' wanakwenda kwenye kazi
Palikuwa jitu juu meza yenye glass
Limeshika tissue kusafisha chemba ya risasiWalijaa na maninja na ma bouncer
Wamevimba wenye sura za kutisha
Wamekausha
Wamegadhibika mpaka amani ilijificha
Nilihisi mkojo unatiririka kwenye trouserSura za kutisha nafuu devils
Crate zimemwaguka utadhani sikukuu kesho
Kulikuwa kumejaa camera full angles
Huku warembo waki-twerk twerk juu ya pool tableHuku watemi wa ngenga wameketi
Mwonekano wa Rostam Bakhrеsa na Mengi
Palikuwa na mabegi ya cheda na chеnchi
Yalikuwa mengi hata wachache kubeba hawaweziWalikuwepo mabinti wamefanya line up
Mfano wa dinner set Sura ziko innocent
Zikionyesha zina majuto ya kusign up
Na baadhi yao walikuwa wadogo yaani minorsBabake Jesca alisimama kwenye chanja
Ametingwa kuchanganya plama kwenye ganja
Nikamsalimia hakuijibu salamu yangu
Akavuta beri kisha akapiga chafya mara sabaKabla muda wake wa kumaliza
Akanyonga jani akapaka mate kwenye Lizzla
Akasnap vidole kuonyesha alikuwa Taita
Kumwita Mrembo na mrembo akaja Na lighterMrembo akamwashia kipuri wakapiga Puff mbili
Wakatoa moshi wakaanza kukiss pasi siri
Ka’ wacheza ngono mbele ya Binti yake Jesca na mbele yangu kiasi nafsi ikakosa tafsiriBaba'ake aka-struggle kukumbuka jina langu
Nikamwambia jina langu naitwa Toni Glove
Akauliza umemjua vipi binti yangu
Nikamwambia mi na jesca tumekutana kwenye coffee shopAkaisogelea glass, akanywa kilichomo kisha
Aka-scan majibu
Ili kuhakikisha ninachokiongea fact, akasema sikujui unatokea wapiNikamwambia nimezaliwa hapa Nonde Sua
Nyumba no 77 kwa mzee Kilua.Akasema ninapiga simu mbili tatu kama hawakujui
Nitakushauri tu uombe duaAkaja mtu akani-snap kwenye IPhone
Design kama anafanya michongo ya passport
Akainua uso nikaona umeweka ndita
Akatikisa kichwa kisha akaendelea ku-type moreMkono wa jesca begani ukinipeti peti
Huku moyo wangu ukienda lesi lesi
Board guard wake wakinichekicheki
Mara wani-search mifuko mara wani-search begiNikaletewa maji ili nipoze kiu
Design hamu ilinikata mzee
Wasaidizi wakingiza jina langu kwenye simu ya kimtandao
Kunifanyia background checkBabake Jesca
Akanipa face look kisha
Akaomba simu sikubisha
Akaanza kukagua photo Akalog in kwenye social kunikagua Facebook TwitterGhafla ukimya ukaitawala nyumba
Wakati akili ikiwaza kufa
Nikitushwa Na yale mandhari yanayofanana na nyumba ya mafia mkubwa
Kutoka Kuala LumpurAkauliza je nipige down town
Maana najua kila mtu kule ukinidanganya bure
Nitakukausha kama kau kau mpaka uta shout shout
Jesca akasema Daddy calm downMi na Tony tayari tumependana
Amekuja kutoa mahari ili tuishi ka' mke na bwana
Anaomba kibali anataka kunioa
Na kama utakubali basi soon tutafunga ndoaBaba Jesca akaegemea kwenye kiti mwisho
Akashusha pumzi kwa masikitiko
Kwanini unadate na mtu hatumjui
Na unajua style ya kuleta hawa wakati ringi
MwikoJesca unajua hadhi ya hii business
Equation ya ndoa haifiti into this case
Kwanini usitafute a guy from inside
Ipo time utaleta ma-spy au ma-witnessJesca akajibu daddy Tony Doctor
PhD holder chuo kikuu cha oxford
Anamiliki migahawa kadhaa hapa town
Analipwa vizuri na kipato kinamtoshaNamfahamu Tony sio mnoko
Na kwao wana uwezo sana baba yake don sio kitoto
Tumejuana miaka kadhaa ameshanikaa
Maana penzi nililolihifadhi moyoni sio kidogoBabake Jesca akanicheki amenuna
Nikawa nimevex nimechuna
Moyo unaenda resi kama duma
Mabaunsa yapo next yametuna
Yakisubiri mechi hii kubumaNikamwona mshikaji ameshika panga bisu
Alikuwa busy anapanga vitu
Sura yake ilikuwa tayari kuanza bifu
Jesca akaniambia yule kaka'angu na ana anger issuesAkaja ameshika vipisi vya kete
Kisha akanidadisi si kibwege
Akashout naskia harufu ya polisi kwa huyu bwege
Jesca akamuwahi akasema we' chizi acha usengeAkatoa syringe kwenye small bag
Akauliza unapendaga cocaine
Nikamwambia huwa situmii hizo zaga
Kaka'angu alitumia akabwaga akajibu okayNilihisi harufu ya casket
Kaka'ake Jesca alihisi mi' shushushu akani-suspect
Nikahisi napokwenda sio
Moyo wangu ukienda mbioBabake Jesca nae anahamaki
Baada ya kugundua nina camera kwenye kifungo cha shati
Akatoa bunduki nikahisi uhai wangu unaishia
Ndipo polisi wenzangu wakavamia
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.