–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

JESUSTA
Dizasta Vina
Hatia II
JESUSTA • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Ah!
Nilipaa sasa natua
Kwenye/kwenye
Siri ya moyo
Na siri ya moyo
Anayeijua mwenye/
Mwenye ujasiri wa
Kutunza nafanya
Ninachodhani ni
Sahihi kitachotokea
Nitajua mbeleWanasema mwanaharamu
Haijui laana/ kashalaanika
Nasikitika kuwa haujui
Kama/ naonekana ka'
Kondoo kwa mchungaji
Lakini...lakini kwa ndani
Mi’ ni chui mamaKwa mfano nakuita mpenzi/
Na tabasamu zuri wakati
Najua kuwa sikupendi/
Kuitoa hii siri ndo' siwezi/
Kwahiyo nitakudanganya
Mpaka ifike siku niutimize
UshenziHuwa nawaza nikuweke
Ufahamu/ mtambue
Kuwa mpo wengi
Na lengo niwateke
Kwa zamu/ niwaumize
Ili mpeleke salamu/
Masikini mrembo
Nashangaa jinsi unavo'ngoja
Pete kwa hamuVile hunioni kwenye
Makundi ya baa/
Na bahati nzuri haujawahi
Kusikia nikizushiwa uzushi
Kitaa/ nakununulia
Rubi kadhaa/ unahisi nakujali
Kumbe unampigia mbuzi gitaaSometimes unanisongea nguna/
Au wali ukidhani mi’ najali ilihali
Sina habari, sina hisia siwazi
Hata kukuonea huruma/
Na sibadili dhambi hata
Mbingu ikisogea nyumaAh!
Nashiriki nawe nyakati
Twitter mpaka instagram/
Picha unani-hashtag drunk in love/
Nanunua brand za gharama za
Hand bag/ perfume kali
Simu ya ghali breakfast
Zanzibar/Haimaanishi kuwa
Tunaianza safari/
Nataka nikuandalie maumivu
Makali/ nahitaji nikuguse
Ili kila unachokiona
Kiwe kinafanya unikumbuke
Ni hatariInaitwa zuia nanga kabla
Bado haijang'oa/
Maana haujaheshimu
Mvua kama bado hujaloa/
Kwa huu mchango ninaotoa/
Ndo' unafanya unazama
Zaidi kiasi unaiwaza mipango
Ya ndoaJicho la tatu hauna
Fungua jicho lako la pili/
Utagundua kila ninachofanya
Kwako batili/ unanipenda mno
Ndo' maana haujaona bado
Dalili/ kuwa we sio wa kwanza
Wala haupo kwenye
Mpango wa pili
Ah!!Unaniletea zawadi toka
Majuu/ kuna wenzio
Nilishawaacha
Na walinichora tattoo/
Mi sio tunda mama...
Mama mi' kidonda
Utachelewa kusonga
Ka' bado unaingoja nafuuSherehe ya birthday yako
Kwenye 'temple' ya anasa/
Umekuwa ’mental’ kwa
Huu mwendo ndo'
Umenasa/
Kiasi unahisi huu ni upendo
Na sasa/ hautambui kuwa
Tukishiriki tendo tu nakuachaKichwa changu hichi,kichwa
Changu kishajadili/ kwamba
Nitalala na wewe na
Wewe na haifiki jumapili/
Nitakuwa nimeshakuacha
Ah! utanitafuta
Kwenye simu ambayo
Namba nitakuwa nishaibadiliUtanitafuta mara mbili/
Mara tatu kisha nne
Utagundua kurudi
Sina dalili/ ngoja ngoja
Itang’ata moyo wako
Kikatili/ mja wa
Watu maumivu
Hukujiandaa kuyakabiliUtanipamba majina ya
Kikafili/ sitasikia maana
Nitakuwa mbali nishasafiri/
Nishasahau utatunga nahau
Kukanda mwili/ na huo
Wakati haukuwahi kuutabiri/
Ila upoUtaumia utashindwa kusimulia/
Utaniulizia kwa wanaonijua
Watakwambia/ kwamba
Hauna tena chako
Okota vipande vya moyo wako
Nenda zako kaandike
TanziaKisha watajua wenzio/
Wanafiki watacheka
Wanaokujali wataangua kilio/
Watakusindikiza kulia/
Watakupa pole wengine watasema
Tulikuambia/ kuwa
Wanaume wote mbwa!!Taswira itazongwa
Na wingu/
Picha utazichoma
Kwa kisu/
Utanitukana mara mwana
Haramu mara malaya/
Rafiki zako wakuu watakuwa
Filamu na riwayaWimbo niliokuimbia
Kamwe hautokukonga/
Utachoma mkuki moyoni
Kisha kunyonga/
Utaendelea kungoja/
Utagundua mvumilivu
Hali mbivu hiyo
Methali iliongopa/
Utagundua ilikuwa
Ni soga/Hii itafanya ukonde
Na kuanza/
Kutumia pombe na ganja/
Nayajua haya yote
Kwa maana ndo nilikotoka/
Utasimama kijasiri
Na mwisho utadondoka/
'sikiliza'Wataleta daktari
Akuulize nini shida/
Hawatapata
Jawabu kabisa/
Wataleta sheikh
Wataleta mchungaji
Wa kanisa/
Watasahau kwamba
Moyo uliovunjika
Hauna tibaNatamani nikuambie kuwa nimekuteka makusudi/
Maana unasikia na hujifunzi/
Nikuumize kama mke wangu mpuuzi/ aliyekimbia na rafiki yangu siku moja baada ya harusiNilishaambiwa na
Mama nikapuuzia/
Kuwa haujawahi
Kupenda kama
Haujawahi kulia/
Kuna muda mtu mbaya
Hutengwa na hatia/
Maana kafiri hazaliwi
Utengenezwa na duniaUkijiua sitakuona
Mzembe amini/
Nitakuvalisha pete
Ruksa uipeleke baharini/
Najua tiba ya
Upweke amini/
Mwisho wako ni
Kuwa kicheche kama
MimiHapo utajua kunihukumu
Sio haki/
Mwanamke kama
Wewe ndio amenifanya
Niwe muasi/
Bila hofu wala
Kiwewe/
Nitaendelea kuzunguka
Kutafuta wasichana
Vipofu kama weweSina hatia ..
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Panorama Authentik. All Rights Reserved.