–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

JESUSTA
Dizasta Vina
The Lost One
JESUSTA • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Alivaa sketi inayoangaza ilikuwa nyepesi
Fupi unaweza dhani ni kidenti
Japo nilikuwa single ila sikuwa mingle
Alizidisha maringo alipogundua namchekiHaiba ya aibu mfumo wa kibinti
Kidogo rangi na lile umbo la kimisi
Akiweka pozi nihakiki
Alikuwa anang'aa ila ngozi yake ilisanifu dhikiBado ilikuwa hainiboi kumtazama
Macho yangu yalikuwa yana-enjoy alichofanya
Kiasili nilikuwa hoi kiasi cha kutogundua alikuwa na konvoi la mimamaKwa mtindo wa kujongea kwa madaha
Yule malaika akaanza kusogea nilipokaa
Hata kabla sijaamua kumchunguza
Macho yaligundua kuwa binti anajiuzaHiyo iliweka ufa moyoni
Nilitamani hata kustuka ndotoni
Kwakuwa nilipata hisia kali za upendo
Nikawa tayari hata kujitupa motoniNilitekwa i only needed her for the rescue
That's how far love can take you
Nikataka mpaka kumvika pete
Awe mchumba nikasahau mwenzangu anawaza cash tuNi aina ya wasichana wanaotokea kwenye ndoto
Yaani unafumba macho alafu unaona anakulelea watoto
Kwa mara ya kwanza maishani mwangu niliwaza ndoa
Hasa baada ya mapenzi ya wasichana wa town kuniboaAkiongozana na kundi la wenzake
Akasogea akitoa sauti za kipambe
Kila mmoja akijinadi kwa mikogo ya mahaba
Nakumbuka mmoja alivua brauzi nimtomaseAlijinadi kama ng'ombe mnadani
Nikataka nijitose chakani
Yaani nijitoe sadaka nilimwona kama kidani cha dhahabu
Maisha ya mjini yalifanya ajione hana thamani
Tukagonganisha macho kihisia
Ndio nikajua nimezama na sijui nitakapoishia
Apendae kipofu nikazisahau kasoro
Nikashuka nikamfungulia mlango akaingiaKwa pupa nikadrive mpaka home
Nilipofika hata kuzima gari sikukumbuka
Kuna muda nilimkuta uchi kitandani
Anauliza kama tunaenda kavu au kwa ndomNikamsihi avae nguo
Akahamaki akauliza maswali mawili kwa mkupuo
Jogoo hawiki braza au ume-mix machaguo
Nikamjibu mi msafiri na wewe binti ndio kituoKwa jicho la kufuga kisasi
Akanicheki kiasi kwamba niliyumba kinafsi
Akanikumbusha hajaja kwangu kutafuta hifadhi
Anafanya biashara na kwangu amekuja kikaziNikashika usemi uchafu ukiingia kwenye kapu toa
Usitupe kapu kwahiyo sikumwona kama changudoa
Nikamwambia nikimwangalia
Kwanza nawaza kujenga pili familia na tatu ndoaHakuitikia akanitenga na himaya ya majibu
Moyo wake haufunguki na ninahitaji rai
Hatukuwa sawa nilitaka kujaribu
Akanijibu Kipepeo na nyuki hawatagi yaiAkaniruhusu kumkumbatia
Akashika mikono yangu akaibusu kwa hisia
Sijui alinipa nini nilijikuta naanguka
Kizunguzungu ile kustuka kumekuchaNiliamka na mawenge kichwani
Nilighafirika kugundua hakwepo chumbani
Aliondoka aliniacha na aibu mtaani
Maana aliposepa alibeba kila kitu ndaniAlikuwa kunguru na nilisahau hafugiki
Hata iwe kibudu kwa nyanya na limao haungiki
Alibeba vipi sijui kinachoniuma
Ni kukosa pendo la huyu bintiSitasahau macho yake mawili ya kirembo
Sauti iliyowasilisha upendo
Akipigwa vikali na ubatili wa matendo
Ya mwili wake mzuri ambao haustahili matesoAliniachia meseji alipoondoka
Akinipa pongezi kwamba sikuwa mwoga
Kuufuata moyo wangu akaniomba msamaha
Akisema hawezi kuenzi penzi ambalo kwa wazazi alikosaSawa ah! Nimekusamehe zamani mami
Pendo lako dawa ewe baniani
Niahidi utawasamehe wazazi wako pia
Ambao wamefanya uonekane shetani honeyI'm kinda lost I do things i ain't suppose to
I thought you'll be my best friend that I can talk to
I wanna change if you wanna change I'll support you
I think we both need the way out that we can walk throughAh popote ulipo ambapo info inafika
Bado mrume nipo miaka inapita nauandika
Huu wimbo umenifundisha nisitue mzigo kama ninahisi sijafikaNaoa kesho na nina hamu kukukuta
Nikwambie dunia safi binadamu ndio uchafuka
Ni kawaida usisahau kutabasamu kukikucha
Nakuombea afya kwenye nyama damu na mifupa
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Panorama Authentik. All Rights Reserved.