LYRICS

Search for a song or choose an album and track.

NDUGU WA MBALI album cover

NDUGU WA MBALI

Dizasta Vina x Kaa La Moto

Shaaban na Ngugi

NDUGU WA MBALI • Dizasta Vina x Kaa La Moto
Lyrics copied!
VERSE I — DIZASTA VINAUjio wa kasi na hadhi ya makombora Kichwa cha kazi, kadhi ya Hifadhi ya tungo bora Jihadi ya kutochoka, hitaji ya tunzo chora Kuona tofauti kati ya miradi hii ya WakoraNa baraka za mababu, sauti inaongea Kwa mahesabu ya dhahabu, ni aghalabu kukosea Ajabu ya hii rahabu, si upatu wa kuotea Na katu sioni tabu hizi tanzu kuzichocheaIlani zina rehema Wachawi wa miji yote ya mbali na ya jirani, imani zinatetema Ghani zinawiwa vyema, zinachapishwa tenzi za ndani Unaweza ukadhani Shaabani kazaliwa tenaMswahili, uhali gani? Ihali gani kani? Ya msukumo wa kujifunza kutunza ilani kali Ya masimulizi na upangaji wa silabi nami Nakusafirisha hadi uhisi nyumbani mbaliHuu ujio ni ishara ya tanzu za maana Kwenye vitivo vya mijadala, sauti yangu ni gharama Nikizuru mihadhara, wanga wanachagama Usiende pao pakavu na pangu pana salamaDarasa linamdadisi mwalimu Linataja na jina ili kuonyesha linasadiki hizi mbinu Kichwa hiki sio kinu Nabusu ardhi kushukuru asili iliyoumba kipawa hiki adhimuMidondoko ya tungo adimu Sentensi zenye misimamo, unaweza sema nyundo ya hakimu Naganga mbele, sisikii jeuri za wadhalimu Napanga herufi na herufi zinaleta tarakimuKwenye hundi Jarada la makada wanasema mi ni fundi Wanajipanga na wanasanda kwa makundi Hakuna msaada wa majani au gamba kichwaniHakuna uchawi, ni ujuvi na ulumbi Kwenye vituo vya sakarani, mi ni mbuji Misamiati hapa imelala kwa mkufunzi Gharama gani kwenye chakula, ila wakatiWa mapishi tunajua chenye thamani huwa ni chumviJumbe zinasafiri ka fununu Tunu ya sentensi ya kikatili ka hukumu Sumu wanajadili, ka kutano la siri Mawakili wanakesha kunikabili ka jukumuStanza zinapangwa kwa vitaru-vitaru Kwa waja wateketeke na vijana barubaru Akili za waruwaru zilishindwa, ni patatifuNyayo zangu zikigusa marumaru Ahh, nimesheheni silaha kama manowari Kila msamiati una uzito wa matofari Ukiona utofauti wa kung’aa na umaridadiTambua mi sio mwenzako, damu yangu samawati Kazi yangu ni harakati, mistari ni sala safi Wabanangaji wote ni mfano wa karimati Ukubwa na ujazo ni mafuta-mafutaUkigusa, ukigusa, utakuta pana hewa katikati Koja la lugha sahihi linakaangiza Fasihi inaimarishwa, utabiri unakamilika Jamii inafundishwa, unabii unakamilishwaHata walobisha wote wanatii, kwa hakika Ukiniona kwenye rununu, penda Fununu zinasambazwa kuwa mimi ni ndio tunu ya malenga Kazi ya kuchochea sukununu na tafitiKufikiri kwa uhuru, huru kwa walengwa Sina wema, ila sio mhuni kwa matendo Kama lulu natafutwa na Warumi wa Efeso Naheshimika na wachumi wa MasakiNasikilizwa na walala hoi wa Buguruni mpaka Keko Salamu wachimbaji, hiki kitalu sahihi Unashikishwa adabu na manju mahiri Anayepambana kuufuta upumbavu wa jijiNa kuleta habari njema ndio yangu nadhiri TwendeVERSE II — KAA LA MOTOHii kalamu ipo huru, nawakata-kata, Kalima Kwa hii fasii ilojaa nuru, Allah, Rasulu, Madina Nashukuru kwa hii zawadi, sitoikufuru, Karima Amini yeye ndiye mpaji, kanipa kipaji, NgirimaKuna siku nitasimamiwa, watu hawatashuka, sijida Acha nifanye leo, hata kesho nikishuka, siji Dar Mtanikumbuka kama mwanazuoni, Nassor Bacho Na sioni wa kunisimamisha, hata kwa mpako wa SabatoMi waziri wa madini kama sultani, Ali Hassani Zanzibari kama Mwinyi, niwekeeni siti yangu Pwani Nguli kama Siti, ongeza tashtiti kuhusu kijiti Au iongeza misamiati, tumbiri kaiona miti?Tafsiri hii, mdomo ni mmoja, masikio mawili Na taarifa ni za mauaji, na vina watazika mwili Kwa kina watajadili, kisha vunda hakina ubani Wakina fulani hawachezi na sisi, tuna roohaniHiki kichwa kimeshinda masheikh na makuhani Malbadiri, majuzuu, marukia na mayasin Bei zimepanda na siuzwi reja-reja Mpaka TMK, wazee wa mapanga, njooni mmoja-mmojaUsinichukulie poa, ama wa ziada tu kama Rashid Nitakukamua, njoo kichwa-kichwa, kula za uso saba Kwa game tumevaa mabomu, kama tunakufa shahidi Niliona bora kuliko ngada ama kuanza kukabaShahada za uzamivu ya heshima, honoris causa Ukiniona kausha, huku unapigika, hata uwe baunsa Mali ka Mansa Musa, tap, maji yanakauka Navuka upande wa pili, halafu namuachia JoshuaBaada ya hii tunaacha alama, niite Tetekuwanga Na bado nina ufalme wangu, na sijabaka Buganda Labda Daudi, kwa PAC hii, nashusha mabigi Goliathi ama King Saul, nakuwa mfalme wa WayahudiMi jabali ka Mwanza, zinasifika Faridi Nilipomzika Qubanda, na nikalijua na jiji Kama Eskimo, sioni wa kunitia ubaridi Hiki kipaji maridadi, mix ya Shaban na NgugiChunga sana ukiambiwa una future na watu wako nyuma Hawaharakishi,watakukalisha ka sumo na Yokozuna Hiki chumba cha upasuaji, tunakosa huruma Kuua marapa ni faradhi, kuwazidi tenzi ni sunnahRapa toka enzi, game halina ushenzi wala Macheda Halina hifadhi, tuzo ya malaika anapewa Makeba Tuna mali, usisahau zawadi alitoa Makeda Saiz zinaumia nyeti, tukiacha madogo washike begaZinapotea vyeti, ukisikiza beti kwa hawa wajuba Kiswahili na fasihi, nahau kama nipo Unguja Nawachenga na lugha, nawavuruga waliokuja Hadi wanasahau kuwa mi ni mbora wa kila mudaNa sijazeeka bado, nipo gado, usilete uchuda Na ikitokea nimekufa, zibaki hadithi na ushuhuda Bado aluta inaendelea baada ya Kaluta, Amir Abedi Na Saadan Kandoro ama Muyaka bin HajjiSijui imekuaje, wachenguaji wamekuwa wachekeshaji Na kule kwengine, mchekeshaji amegeuka mcheguaji Ni kazi kubwa kama kuishi na samaki nje ya maji Na tusipochunga, vipofu watageuka watazamajiHe baba, tupe hifadhi, kalamu zinaisha wino Tunakosa mahujaji na elimu ya mtaani ka D Knob Wengi wanakata viuno, usininukuu vibaya Chino Kwa kuwa nyie ni singers, cherehani kuna mishonoTungo zina flip-flap nyingi, Rivellino Unaweza zig-zag ama keep it straight, Gogo Simo No elastico, first kwenye list, last siko Naandika ninachokipenda, maandiko, Steven BikoHatupo kwenye sakata, nani mbora kuliko huyu? Tunaishia kujitukusa badala ya kutukusa Mbuyu Kusudi ni moja, azma ni moja, kufikia nduyu Kupata mapene, usije kuhurumisha ukifika MbuyuTangu maa, baa na irabu, toka vidudu Mpaka maabara, semi na tenzi, zote namudu Niko too proud kwa hii kitu, naifanya kama sugu Level za Ki-Taita, kabla sijakua, chakula cha waduduWatunzi wananiogopa, nitatoa siri kama dudu Na sio juu ya pombe, zinatunzwa asili kama juju Chini zimelala diamond, juu daymond kama Fubu Jini huria, mi ni adili, naomba uwasamehe nduguHaya, mnikome mfugaji, zizini mbuzi hatushindani Hapa kazi juu ya kazi, mjomba, hatushindi ndani Na uwaambie watoto wadogo pia, hatuishii ndani Nawapa joto, hata kama sote tuna-share faniNimekuwa classic toka minor, kageni kwa mchezo Kwa haya maelezo, sioni wa kunizidi kwa mchezo Juu kileleni, so keleleni, zimelala Kibo Napaa juu uhuru, si kaa tai juu, egoNashukuru nilichonacho, na pia nashukuru ambacho sina Najua nitaipata kesho, cha muhimu leo nipo mzima Kama uliskia wanatema, jua sio tamu yao Ama amesifiwa mgema, sasa wamelitia maji tembo lao

More From This Album

More songs from this album

Join The Family

New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.

© 2026 Dizasta Vina. All Rights Reserved.