–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

THE VERTELLER
Dizasta Vina
A Confession of a Mad Philosopher (feat. Dash)
THE VERTELLER • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Maana ya uhuru huisha baada ya utambuzi
Baada ya kutambua kwamba uhuru si maamuzi
Maana Kifungo na mipaka vinafanana
Aliyekuambia kuna uhuru utaupata kakudanganyaIpo asili inayofanya mwili wako mashine
Kufanya Ugonjwa uwe jela alafu afya ni jela nyingine
Mjamaa amemwaga damu tayari
Awe huru ili akawe mtumwa kwa mabepariChagua kufa ukiona waja hawalipi wema
Kufa wokovu kilichokufa hakifi tena
Kufa ni uhuru kamili tabu ni nini
Haupo huru sasa uhuru wa kweli ni kaburiniUnakumbatia uhuru wa kuambiwa
Wakati unaishi na haukuchagua kuzaliwa
Uhuru hautafutwi msafiri pumzika kubali chai
Hauwezi kuwa huru ungali haiUhuru si halisi jamaa badili umbo
Uhuru sio jibu hata usikariri fumbo
Uhuru ni falsafa ya vitabu iliandikwa na mababu
Tutaisoma na mwisho itabaki hukoAnayehitaji uhuru aelewe
Kuogopa kufa ni utumwa kwa maana kufa ndio uhuru wenyewe
Hata uwe mfalme ambaye anatoa idhini
Huwei kuwa huru uhuru wa kweli ni kaburiniFreedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedomUkikumbatia mwanga jua utaificha nuru
Uhuru si kwa mwafrika kumkimbiza mkabulu
Kuutaka uhuru sana jamaa si dalili njema
Kama upo hai na unahisi uko huru fikiri tenaCheo huleta nuru pahala nuru haifiki
Na pesa ndio njia ya uhuru ukiimiliki
Pesa na cheo upita kule hakuingiliki
Alisema mlevi mmoja ambaye pombe tu imemdhibitiMwathirika ambaye dawa za kulevya zimefunga
Na anahisi yuko huru mara baada tu ya kuvuta
Labda si kweli haupo huru ukijiongeza
Maana ukishaujua uhuru tayari ushaupotezaJe utaniona chizi au mwivi
Au pumbavu au mshenzi ninayeongea vituko
Au utaamua ukae chini utafakari
Kisha ukakubali ndoa ajira navyo pia vifungoAliye huru ni nani nieleze mtoto anayeenda kwa viboko
Au mlokole mtenda mema baada ya kutishiwa moto
Au msomi elimu mpaka chuo kuhakiki
I swear kama uhuru ndio huo siuafikiAnayehisi yuko huru pita mbele
Piga kelele maana hata Mungu wako hayuko huru
Hawezi kubadili mipango hawezi kumuumba
Mungu mwingine mkubwa kupita yeyeUnaetafuta uhuru wa kweli utateseka
Utapoteza damu utatoa machozi na utakesha
Hauwezi kuupata maana hakuna ulipouweka
Uhuru haupatikani kwa fedhaUhuru is priceless kwakuwa si bidhaa halisi
Wenye chapaa walihakiki
Utaniangusha sana ukishindwa kuamini
Upo uhuru ila uhuru wa kweli ni kaburiniYou've got no freedom
You've got no freedom
You've got no freedom
You've got no freedomFreedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
Freedom freedom
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Panorama Authentik. All Rights Reserved.