–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

THE VERTELLER
Dizasta Vina
Kibabu Na Binti
THE VERTELLER • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Mhoji: “Mmhh… kwahiyo ni nini kilikujia akilini aah!! mara ya kwanza ulipomuona kibabu?”Binti: “mh….Pesa, eeh! Pesa. Suti aliyovaa, gari anayoendesha, vyote viliongesha kuwa ana pesa”Mhoji: “aah okay..!! Sasa ina maana hukujali vitu vingine?”Binti: “ mhh! Hapana. Umri, background yake, kazi yake, havinihusu. As long as ana pesa”Msimuliaji:Ah
Binti akaweka pozi matata
Kibabu akaona huu ni msosi akaja
Binti akamkonyeza kibabu, kibabu akajibu
Kibabu akafungua pochi binti akiifungua zipuBinti akavua nguo zake za mwili akideka
Akimwacha yule kibabu tajiri akitweta
Hakujali kuitwa malaya hakuona haya
Kwa maana akili yake iliwaza pesaAkathibitisha kibabu ana sumni za kutupa
Alikuwa na mvi kuonyesha umri pia ni mkubwa
Akajisemea “kibabu anafaa kuwa baba yangu
Ni ajabu kuona anapiga tour kwa machangu”Akaendelea kuwaza “labda pengine hana mke
Kwamba ndo’ maana huu utamu anaufata nje?
Au mkewe ni mvivu utamu anaupata nusu?”
Akaacha kuwaza baada ya kugundua hayamuhusuBinti akalikabidhi tunda
Ilikuwa shughuli kamili shahidi kuta
Alijituma kuigiza furaha ilipobidi
Aishinde dhiki maana babu alimuahidi bundaBinti akaweka mashauzi ki-star mpaka
Kibabu akaenda round kadhaa hata
Vyumba vya jirani wote walishtuka
Kumsikiliza babu anatoa sauti za raha ah!Na sisi mashahidi tulikuwepo
Na hii ndio inafanya hii hadithi iwe special
Binti aliwaza leo, hakuikumbuka jana na upeo wake
Haukumruhusu kuitabiri keshoMhoji: “aah okay kibabu”Kibabu: “mh ndiyo”Mhoji: “Kwanza naruhusiwa kukuita kibabu? Maana najua hilo sio jina lako halisi”Kibabu: “ heh! He heee! Aah Hapana shida, hapana shida nimekuwa nikiitwa hilo jina kwa muda mrefu na vijana wananitania…kwahiyo hakuna shida unaweza tu ukaniita kibabu”Mhoji: “Mh okay basi nitakuita kibabu na nilitaka kujua ni kawaida yako kuwa unanunua hawa madada wanaojiuza au ni mpenzi wa kutembelea haya maeneo mara kwa mara?”Kibabu: “mmmh! Kwakweli siwezi kusema ni tabia yangu, mhh hapana, japo nimefanya mara mbili mara tatu. Siwezi kusema nafanya ninafanya hivyo mara kwa mara kwamba ni tabia yangu lakini ni….Ukishaoa utajua kwamba kuna muda ndoa ina changamoto za hapa na pale…alafu uta.. unafahamu wewe ni mwanaume”Msimuliaji:Ah! Kibabu akaliona pozi matata
Kwakuwa ana noti hakuona ugomvi kumfata
Kibabu akakonyezwa kibabu akaji
Akaifungua pochi kuona binti akiifungua zipuKibabu alitokwa na mate
Hata noti zilizomtoka si chache
Hakufikiri ada za watoto za masomo
Alisahau yote kwa maana ubongo uliwaza ngonoAkamtazama yule binti maridadi
Akajiuliza “vipi kaichagua hii kazi”
Na umri wake ni mdogo anaweza kuwa binti yangu
Ni ajabu kuona ngono anashiriki na vibabu” ah“Ah au labda ameondokewa na wazazi!
Au wapo ila amelelewa kijambazi
Au hali ngumu au usawa hauruhusu?”
Akaacha kuwaza baada ya kugundua hayamuhusuKibabu akaonyeshwa njia ya mwezini
Akampamba binti pesa ka’ Malkia enzini
Alikuwa ka’ karogwa raha zilimzonga bila
Uwoga akajitosa kuingia penziniAh na sisi tuliosimuliwa tuliokuwepo
Ndio inayofanya hii hadithi iwe special
Babu aliwaza leo hakuikumbuka jana na
Umri wake ulifanya asitake kuiwaza kesho
Ah!Mhoji: “Mh!!! Mhu! Okay!? Okay!! Okay!! Mmh mnaniacha njiapanda!! Eeh…
Na hivi ni lini hasa mlikuja kugundua kuwa ninyi ni mtu na binti yake!??”Binti: ……
Kibabu: ……
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Panorama Authentik. All Rights Reserved.