–
LYRICS
–
Search for a song or choose an album and track.

THE VERTELLER
Dizasta Vina
Muscular Feminist
THE VERTELLER • Dizasta Vina
Lyrics copied!
Dear boys dear… menNi sisi wasichana kina dada, mabinti na mama zenu
Tunaongea kutoka upande wa chini, upande mbali upande kutoka usawa wenuUpande nilipo msichana kuna hitilafu
‘So’ sikio lako thabiti ni ushindi kwangu
Ninayotaka kusema hapa sio siri katu
Ili ujue nina vingi vya ku-offer kabla ya mwili wanguKwa miaka mingi nimeishi gizani
Gizani kwenye baridi na miba mingi nyikani
Eneo uliotaka niishi ni eneo kandamizi
Na bahati mbaya we’ ndo’ mchoraji wa hii ramaniRamani inamwonyesha binti kama chombo cha mapenzi
Msindikizaji mtoto tegemezi
Ramani isiyojua vituo
Isiyojua tunaweza kuwa marafiki bila kuvuana nguoDear boys, dear menMngeelewa mngeiweka fikra sahihi
Kama sanaa jinsi inavyozalisha fasihi
Mi’ ni mlezi ukinivika mi’ umeivika jamiiU-gentlemen sio kulipa mgahawani
Umeshapitwa na wakati
Hainisaidii kunifungulia mlango nikifika kwenye gari
Nifungulie fikra nitafakariDear boys, dear menTumekuwa tegemezi maana mmeficha mbegu
Nani wa kuipigana vita yetu
Umbali kati yetu utakuwa mkubwa milele
Maana si ni wahanga wa mifumo mliyoiunda wenyeweNikijaribu kusoma nabaki bure
Maana unajali mwili wangu, ndo’ maana sitaki shule
Kila nikienda popote wanaomba ngono
Labda niwe changudoa to the fullest
At least I’ll get paidHata sisi tuna life too
And the world doesn’t revolve around you
Nipo tofauti sikupenda, na tena
Unaponichezea fahamu kuwa ninazeeka mapemaShujaa unakumbukwa mzazi sikumbukwi
Na kwanini kuwa msafi sio haja kwako
Au kutembea kifua wazi ni kujiamini
Nikitembea mimi ni nusu uchiI wish ungejua pride yako nayo sumu
I wish ungejua kuwa uanaume sio nguvu
I wish ungejua kuwa binadamu hajakamilika
Mwanaume aliyekamilika anatimiza majukumuI wish ungejua kuwa na mimba sio haya
I wish ungejua mwanamke kuwa kichwa si vibaya
I wish ungejua kuwa upendo nao una nguvu kwahiyo mwanamke akitongoza mwanaume si malayaI wish ungejua kuonyesha fear sometimes, it’s okay
It’s okay kulia sometimes
I wish ungejua uongozi hauoni jinsia si
Tatizo mwanamke kuongoza njia sometimesMifumo mliyoianzisha ina maisha
Na chenye maisha kinazikwa
Kwahiyo ipo siku mwanamke atasimama
Na vita tunayopigana tutashindaInasikitisha hamkui kihisia, japo mnakua kiakili
Natamani … natamani mngejua kuwa inauma sana kuwa namba mbili kwenye kila nyanjaEgo ni power ila iogope
Maana ni upanga unaokata pande zote
Ngoma nzuri ngoma nzuri haitavuma milele
Ukitumia ubabe vibaya utakuvunja mwenyeweHadithi ya mwanamke alimshawishi Adam kula tunda
Iliandikwa na wewe
Sijui Delilah alichukua nguvu za mumewe akaziuza
Iliandikwa na weweUpande wangu wa hadithi haujasikilizwa
Pengine hautasikilizwa hasirani
Maana ulianzisha shule akasoma mwanaume
Mwanamke nikabaki nyumbaniDear boys, dear menHamtakaa kwenye kilele
Maana kilele ni kuwa mama
Mi’ ni kichwa sio wewe ungekuwa kichwa
Mtaani kusingekuwa na single mothersLini mtaacha kutuita mademu
Au labda mwite demu mama’ako
Ukiona hauwezi naomba niheshimu kwa maana heshima inaanza kwakoNa haja ya maelewano iko hapo
I mean… ipi salama ya kichwa cha familia bila
Mkono wa kuosha macho?Najua tupo tofauti
Na tofauti yetu itabaki, itabakia hivyo milele
Ila naomba usinichukie nieleweDear boys, dear menNi sisi wasichana, kina dada, mabinti na mama zenu
Tunawasilisha kutoka upande wa chini upande wa pili
Upande mbali kutoka usawa wenuDear girls, dear WomenNi sisi kina kaka, kina baba, wanaume machizi wenu
Tunaongea kutoka upande wa juu, upande wa mbali
Upande uliowekwa na asili yetuUpande wenye mafungu yenye ulanguzi
Upande wenye uthubutu na maamuzi
Upande wenye machozi jasho na damu
Uongozi upako ufahamu, upande usio na uhuru na uchaguziUpande uliofanya wanaume tutengwe na tunu
Tutengwe na tunu
Upande ambao pengine kuishi wewe ni ngumu
Upande ambao asali yake ni kilele cha sumuUpande ambao haushabikii tija ya upendo au furaha au amani
Kama hauangalii pima utagundua upande niliosimama mimi ni ngao ya jamii nzimaUanaume sio ushindi ni jukumu
Uanaume sio rizki ni hukumu
Ungejua kwanini wanaume wana msongo wa mawazo pengine ungefurahia udogo wakoDear women , dear girlsMmekuwa chombo cha ngono
Maana mmetufanya chombo cha fedha
Kama nguo hazitabadili mishono
Hatuwezi kuwa marafiki bila ngono nawaelezaMnapoona padogo pana taswira ndefu
Kiasi haujui si ndio tuliopigana vita yenu
Hata mkiamka mmekuwa wanaume leo
Mtagundua kuwa jinsia sio cheoWapendwa tukishindana mtashindwa
Hata mkishinda ushindi wenu hautalindwa
Kama ambavyo kila mmoja anatumia choo chake
Kila mmoja a-play role yake na awe bingwaDear womenNdoa sio mafanikio
Kuna wengi wanakonda maana ndoa zao sio
Ndoa ni mwiba usijivune
Ukiipata niamini unaweza kukamilika bila mumeDada baki shule bila elimu utateseka
Ukitegemea urembo ipo siku utazeeka
Kama ukiweka mwili wako hisani
Ukizeeka tutajali ulichonacho kichwani‘Skiza’ hata wanaume tuna doubts too
And this world doesn’t revolve around you
Tuna stress zinatufunga na tena
Kazi zetu ni ngumu ndo’ maana tunakufa mapemaKama unahisi upo huru umepotoka
Hauwezi kuwa huru wakati umelipiwa posaDear womenIt’s okay kuwa namba mbili
Majukumu sio mashindano acha kukaliliIt’s okay kumlea mwanaume asiye na kazi
Ukaendelea kumuheshimu bila kumshusha hadhi
Mbona sisi tunalea wanawake masikini wamekata ringi na bado mtaani hatutatangaziMwanaume ana jukumu la kujenga msingi?
No, msingi unajengwa na elimu
Kwa mfano nani anayekubali kucheza uchi kwenye videos? Jiheshimu nikuheshimuUrembo pia ni power, ila ni power na iogope
Maana ni upanga unaokata pande zote
Ngoma ya uzuri haitovuma milele
Ukiutumia urembo vibaya utakuvunja mwenyeweI wish ungejua unachowaza ni muhimu
Ukifanyia kazi na kuwa wa kwanza si’ majibu
I wish ungejua kwamba asili imenipa umwamba
Nikulee, kukulea wewe ni msaada si’ wajibuI wish ungejua tuko tofauti hata utunge dini
Hauwi mwamba kwa kumweka mwanaume chini
I wish ungejua kuwa kichwa ni hukumu
Maana hakuna kinachotisha kama jukumuWangapi tumelelewa na hao single mothers
Maskini and we turned out just fine
Maybe idea ya kuacha kujali mtoto sababu
Baba mjinga ingeachwa far behindTunasubiria uhalisi ubadilike
Labda uhalisia haubadiliki huu
Labda ni wakati wa kukubali ili yaishe kwamba
Mtoto ni wa mama na baba ni rafiki tuLini mtaacha kutuita madanga ma-sponsors? Ndio, niheshimu nikuheshimu nitaacha wewe
Ukiona imetosha, au sio?Najua tuko tofauti
Na tofauti itabaki hivyo milele
Usinichukie nieleweDear girls, dear womenNi sisi kina kaka kina baba, wanaume machizi wenu
Tunawasilisha kutoka upande wa juu, upande mbali uliowekwa na asili yetu
More From This Album
More songs from this album
Join The Family
New music. Stories. Early access. Things you won't find everywhere else.
© 2026 Panorama Authentik. All Rights Reserved.